5.1 Vikwazo vinavyowezekana na mikakati ya kushinda vikwazo

Kama ilivyoangaziwa katika sura ya 1, ujumuishaji wa teknolojia za kidijitali katika huduma za Utengamao una faida nyingi kwenye mfumo wa huduma za afya katika Afrika Mashariki, ikijumuisha uwezo mkubwa wa huduma za Utengamao Kidijitali. Licha ya faida nyingi, kuna vizuizi ambavyo vinaweza visiwe vya asili lakini vinaweza kutokea katika matumizi ya teknolojia ya dijitali. Hii inaweza kusababisha huduma za Utengamao Kiditali kushindwa kufanyika ipasavyo, wataalamu wa huduma za utengamao/wateja kukosa motisha wa kutumia, jambo ambalo linaweza kudhoofisha ufuasi wa huduma za utengamao na hivyo kuleta athari.

Orodha ya vikwazo haiwezi kuwa kamilifu. Ukiwa unatumia huduma za Utengamao Kidijitali, ama unapanga kuitumia/kuitekeleza au tayari unaipokea kama mteja, unaweza kuona vizuizi vingine. Vizuizi vilivyoorodheshwa ni vile vinavyotajwa mara kwa mara katika fasihi kuhusiana na huduma za Utengamao Kidijitali katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara. Vizuizi vingi vilivyowasilishwa katika sura hii vinatokana na ukaguzi wa upeo uliofanywa kama sehemu ya mradi huu. Unaweza kutazama usajili wa jarida  kupitia kiungo hiki: https://osf.io/xyvmj [1]. Jarida kamili linatarajiwa kuchapishwa mwishoni mwa 2024.

Kumbuka: Mikakati iliyoorodheshwa hapa chini inaweza kuwa njia za kuondokana na vikwazo vinavyoweza kutokea, lakini itahitaji ushirikiano kati ya serikali, watoa huduma za afya, watengenezaji teknolojia, na jamii ili kuendeleza masuluhisho endelevu na yanayofaa kitamaduni ambayo yatashinda changamoto hizi.

5.1.1. Upatikanaji wa mtandao

Tangu uvumbuzi wa mtandao na uzalishaji wa tovuti ya kwanza mwaka wa 1990, imeendelea kukua kwa kasi ya haraka sana. Sasa hatuwezi kutengeneza upatikanaji wa taarifa yoyote bila kuzingatia wakati na mahali, lakini pia tunaweza kufanya miamala ya benki na kutoa huduma za utengamao mtandaoni.

Mchoro wa 1 unaonyesha ongezeko la watumiaji wa mtandao kutokana na uvumbuzi wa tovuti ya kwanza mwaka wa 1991 hadi 2023 [2].

RADIC swahili 3.

Mchoro wa 1. Watumiaji wa intaneti duniani kote kutoka mwaka 1990 hadi 2023.

Kufikia 2023, idadi ya watumiaji wa mtandao ni milioni 5.158 ulimwenguni kote. Hata hivyo, kuna utofauti wa wastani wa matumizi duniani kote ikilinganishwa na matumizi katika Afrika Mashariki. Kwenye mchoro wa 2 unaonyesha kuasiliwa kwa mtandao mnamo 2023 ulimwenguni kote [2].

RADIC swahili 4.2

Mchoro wa 2. Upitishaji wa intaneti duniani kote, picha imetoholewa kutoka kwa layerace kupitia Freepik.

Idadi ya watu ambao hawatumii mtandao katika Afrika Mashariki ni milioni 328.9 (takwimu 3) [2]. Kuna sababu kadhaa kwa nini watu wengi katika Afrika Mashariki hawatumii mtandao. Kwa upande mmoja, watu wengi hawana pesa za kupata mtandao na kwa upande mwingine, usambaaji wa mtandao hauna mashiko katika baadhi ya mikoa katika eneo hili.

RADIC swahili 4

Mchoro wa 3: Watu ambao hawatumii mtandao ikilinganishwa duniani kote; picha iliyochukuliwa kutoka layerace kwenye freepik.

Kwa vile muunganisho wa mtandao na usambaaji ni muhimu kwa ufikiaji sawia wa huduma za Utengamao Kidijitali, hii inaweza kupunguza matumizi. Hata hivyo, kuna baadhi ya njia za kupunguza changamoto hii sasa na/au katika siku zijazo:

Huduma za kidijitali bila muunganisho wa mtandao

Huduma za kidijitali ambazo zinawezekana bila muunganisho wa mtandao zinaweza kutumika katika huduma za utengamao za mbali. Kwa mfano, ujumbe mfupi unaweza kutumika kutoa taarifa kuhusu hali kama vile mfadhaiko/kisukari na kutoa usaidizi wa kihisia bila hitaji la mtu aliyeathiriwa kutembelea kituo kinachofaa [3,4]. Ujumbe mfupi pia unaweza kutumika kuwahamasisha wateja kufanya mazoezi yao nyumbani na kuwakumbusha miadi ijayo [5]. Kwa hakika, ufanisi na uwezo wa kuboresha huduma za ujumbe mfupi kwa ajili ya huduma za utengamao ni haba. Kwa hivyo, mbinu bora itahusisha kupanua usambaaji wa mtandao.

Uingiliaji kati uliochanganywa

Mkakati mwingine unaweza kuwa ni kutoa huduma ya uingiliaji kati uliochanganywa, kama ule uliopendekezwa na Yusuhp na wengineo [6]. Uingiliaji kati uliochanganywa ni uingiliaji kati ambapo vikao vya ana kwa ana hutolewa katika kituo cha utengamao/hospitali na hivi huchanganywa na vipindi vya kidijitali vinavyoweza kufanywa kwa mbali [7]. Hii ina maana kwamba mteja halazimiki kutegemea huduma za kidijitali pekee ikiwa, kwa mfano, mteja anaishi katika eneo ambalo huduma ya mtandao ni haba.

Uingiliaji kati usiolingana

Ikiwa mteja au mtaalamu wa huduma ya utengamao hawezi kufikia hudumu za mtandao na kwa hivyo uingiliaji kati wa kidijitali unaolinganishwa kama vile mikutano ya video haiwezekani, suluhu nyingine inaweza kuwa ni kutoa maudhui ya huduma mtengamao yasiyolingana kidijitali. Hii ina maana kwamba mtoa huduma ya utengamao si lazima awe mtandaoni kwa wakati mmoja na mteja. Kwa njia hii, maudhui yanaweza kuhifadhiwa mtandaoni na kufikiwa na mteja kwa wakati mwingine kwa mbali. Katika mfano uliowasilishwa na Osborn na wengineo [8], wanafunzi wa shule ya upili walio na dalili za mfadhaiko wanaoishi Kenya waliweza kufuata uingiliaji kati kupitia programu ya kompyuta ambayo inaweza kufuatiwa na wanafunzi katika shule wanayosoma. Uingiliaji kati ulijumuisha shughuli za kusoma na kuandika kuhusu dhana 3: ukuaji wa mawazo, shukrani, na uthibitisho wa thamani. Uingiliaji kati ulizalisha kupungua zaidi kwa dalili za unyogovu.

Uwekezaji katika miundombinu

Serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali na mashirika ya sekta binafsi yanaweza kuwekeza katika kuboresha muunganisho wa mtandao na upatikanaji wa umeme katika maeneo ambayo hayajahudumiwa. Hii inaweza kuhusisha kupanua ufikiaji wa miundombinu iliyopo au kupeleka teknolojia mbadala kama vile nishati ya jua au mtandao wa setilaiti.

Kusaidia kidijitali. 

Mipango ya kisiasa ambayo pia inakuza uwekaji digitali katika nchi za Afrika Mashariki, kama vile upanuzi wa muunganisho wa mtandao na/au uundaji wa miundombinu ya kidijitali ni muhimu ili kufikia huduma za kidijitali.

Kwa mfano, serikali ya Kenya imebuni mpango mkuu wa kidijitali [9] ambao unanuia kujenga mfumo ikolojia wa kidijitali thabiti, salama, wa bei nafuu, unaoweza kufikiwa na unaotegemewa, ambao unanufaisha sekta ya umma na ya kibinafsi, na kuboresha ubora wa maisha hadi 2032. Mkakati huu unaangazia mbinu ya kina ya kuimarisha mfumo ikolojia wa kidijitali wa Kenya, ikijumuisha upanuzi na uboreshaji wa miundombinu ya kidijitali, huduma, bidhaa na usimamizi wa data. Inalenga kuimarisha ujuzi wa kidijitali kwa idadi ya watu, kutoa usaidizi kwa biashara, na kuunda sheria na kanuni ili kuwezesha uwekaji digitali kote nchini. Shughuli zilizoelezwa hazilengi tu mfumo wa huduma za afya bali zinashughulikia sekta zote ambazo zimeathiriwa na uwekaji digitali. Mpango huo bado haujatekelezwa kikamilifu na/au kutathminiwa, lakini unaonyesha kuwa serikali inaunga mkono uwekaji digitali na kukuza miradi ambayo ina lengo sawa.

Nenda kwenye sura ya 4, ili kujifunza zaidi kuhusu hatua mahususi ambazo Kenya, Tanzania na Rwanda huchukua ili kuboresha miundombinu ya kidijitali katika nchi hizi.

5.1.2. Upatikanaji wa vifaa vya kidijitali

Huduma nyingi za Utengamao Kidijitali hutolewa kama programu au kama programu inayotegemea wavuti. Kifaa kinachofaa kinahitajika ili kufikia programu hizi za tiba na mafunzo. Simu mahiri mara nyingi hutumiwa kwa kusudi hili, kwani zinaweza kubebeka na kwa hivyo zinaweza kutumika bila kujali eneo. Hii ni faida kubwa ikilinganishwa na kompyuta au kipakatalishi. Idadi ya watumiaji wa simu janja inaongezeka duniani kote, kama mchoro wa 4 unavyoonyesha [10]. Kwa mujibu kwa utabiri, tayari kutakuwa na zaidi ya watumiaji bilioni 5 kufikia 2028.

RADIC swahili 5

Mchoro wa 4: Idadi ya watumiaji wa simu janja duniani kote kuanzia 2013 hadi 2028 (katika mamilioni).

Pia kumekuwa na ongezeko la watumiaji wa simu janja katika eneo la Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara (takwimu 5), ingawa idadi inasemekana kuwa milioni 688.89 pekee [11]. Hata ingawa idadi ya watumiaji imeongezeka sana katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, kwa sasa si kila mtu ana simu janja  ya kufikia huduma za Utengamao kidijitali na/au pesa za kununua vifurushi ili kufikia intaneti.

RADIC swahili 6

Kielelezo cha 5: Idadi ya watumiaji wa simu janja katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kuanzia 2011 hadi 2028 (katika mamilioni).

Ufikiaji kupitia shule

Kwa kikwazo hiki kinachowezekana, ufikiaji wa uingiliaji kati wa kidijitali unaweza kuundwa kupitia vitarakilishi/kompyuta ambazo wateja wanaweza kufikia. Kwa mfano, itawezekana kwa wanafunzi kutekeleza afua za kidijitali kwenye kompyuta ya shule wanayosoma, kama ilivyoelezwa katika mfano na Osborn na wengineo. [8]. Hii itawaruhusu wateja kufaidika na manufaa ya uingiliaji kati wa kidijitali bila kumiliki kifaa cha mkononi au kuwa na kitaralishi/kompyuta nyumbani.

Ufikiaji kupitia jamii

Mbinu nyingine ni kuwapa weledi wa huduma za utengamao vifaa vinavyohitajika (kama vitarakilishi) ili kuleta uingiliaji kati wa kidijitali kwa jamii. Mfanyikazi wa kijamii ambaye anatembelea jamii mara kwa mara anaweza kuuliza juu ya mahitaji ya huduma za utengamao kwenye jamii yanayohitajika. Hata bila ufikiaji wa kudumu ya mtandao, uingiliaji kati wa kidijitali unaweza kuhifadhiwa kwenye kitarakilishi cha wafanyakazi wa kijamii na unaweza kutolewa kwa watu wanaoishi katika jumuiya hii. Kwa njia hii, uingiliaji kati haukuweza kubinafsishwa lakini unaweza kushughulikia mahitaji makubwa ya jamii.

5.1.3. Masuala ya kiufundi

Kizuizi kingine ambacho kinaweza kupunguza matumizi ya huduma za Utengamao Kidijitali shida za kiufundi katika mtandao au simu janja. Kwa mfano, simu janja inaweza kuharibika au urekebishaji wa kifaa unaweza kuchukua muda mrefu, kumaanisha kuwa mteja hana tena simu janja. Kwa kuongeza, kuharibika kwa seva au kukatwa kwa umeme ni kawaida zaidi katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, ambayo inaweza pia kuathiri vibaya matumizi.

Chaguzi za teknolojia ya chini

Katika maeneo ambayo seva huwa na hitilafu na kukatika kwa nishati ni kawaida zaidi, itakuwa vyema kutumia chaguo za teknolojia ya chini kama vile majukwaa yanayotegemea ujumbe mfupi au mifumo shirikishi ya majibu ya sauti ambayo inaweza kufikiwa kwa simu rahisi za mkononi. Angalia mfano bora wa mazoezi kutoka Teriö na wengineo [12] katika sura ya 2, ambapo kikundi cha utafiti kilitumia huduma za ujumbe mfupi kama uingiliaji kati nchini Uganda ili kuboresha shughuli za kimwili kwa watu wenye kiharusi.

5.1.4. Ujuzi wa kidijitali (afya)

Miongoni mwa tafiti 17 zilizojumuishwa katika mapitio ya upeo yaliyofanywa kama sehemu ya mradi wa RADIC, sita zilitathmini vikwazo na wawezeshaji wa kutumia huduma za Utengamao Kidijitali katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara. Tafiti hizi zote zilibainisha ujuzi mdogo wa kidijitali (afya) wa wateja na wataalamu wa utengamao kama kikwazo kikubwa cha kutumia huduma za Utengamao Kidijitali.

Ujuzi wa kidijitali ni uwezo wa mtu binafsi kupata, kutathmini na kuwasilisha habari kwa kuandika au kutumia majukwa ya mawasiliano ya kidijitali. Ni mchanganyiko wa uwezo wa kiufundi na kiakili katika kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano kuunda, kutathmini na kushirikisha habari. Ingawa ujuzi wa kidijitali hapo awali ulilenga ujuzi wa kidijitali na kompyuta za kujitegemea, ujio wa mtandao na matumizi ya mitandao ya kijamii umebadilisha baadhi ya mtazamo kwenye vifaa vya mkononi. Ujuzi wa afya dijitali hurejelea uwezo wa kutafuta, kupata, kuelewa na kutathmini taarifa za afya kutoka kwa rasilimali za kielektroniki na kutumia ujuzi huo kushughulikia au kutatua tatizo la afya [13].

Kwa teknolojia na maendeleo ya hivi majuzi, kwa mfano, katika mitandao ya kijamii na vifaa vya watumiaji wa simu, mahitaji ya ujuzi wa kidijitali pia yanabadilika kila mara. Hii ni pamoja na kuelewa jinsi ya kutumia vivinjari vya wavuti, vipengele vya vifaa vya mkononi, injini za utafutaji, barua pepe, usindikaji wa maneno, wikisi, blogu, michoro, video na programu ya uwasilishaji. Pia inajumuisha uwezo wa kutathmini rasilimali za mtandaoni kwa uaminifu wa habari. Ikiwa ujuzi wa kidijitali (afya) katika jamii ni mdogo, ni vigumu kutekeleza huduma za Utengamao Kidijitali, kwani mteja na/au wafanyakazi wa huduma za utengamao wanaweza tu kutumia vifaa kwa kiasi kidogo.

Msaada wa kiufundi

Kutoa usaidizi wa kiufundi unaoendelea kwa watoa huduma za afya na watumiaji ni muhimu kwa kutatua masuala ya kiufundi na kuhakikisha utendakazi mzuri wa mifumo ya Utengamao Kidijitali. Hili linaweza kufanywa kupitia meza za usaidizi, mabaraza ya mtandaoni, au timu maalum za usaidizi. Hata hivyo, hili ni suluhu la muda mfupi tu, na mkakati endelevu zaidi ungeleta matokeo bora.

Mafunzo

Kutoa mafunzo kwa wafanyikazi wa afya na wanajamii juu ya jinsi ya kutumia majukwaa ya huduma za Utengamao Kidijitali kunaweza kusaidia kushinda kizuizi hiki. Hii ni pamoja na mafunzo kuhusu ujuzi wa kimsingi wa kidijitali pamoja na ujuzi mahususi unaohusiana na kutumia programu ya urekebishaji kama vile kupokea na kutuma ujumbe mfupi wa maandishi, kutafuta taarifa muhimu kwenye mtandao na kupakua masasisho ili kudumisha usalama wa kifaa, n.k. Hii itakuwa muhimu kwa watu wote, kwani vifaa vya dijiti vinaweza kutumika kwa madhumuni mengi. Programu hizi zinaweza kutolewa kupitia vituo vya jamii, shule, makanisa, na mashirika mengine ya kijamii.

Msaada rika

Kuwafunza wanajamii kunaweza pia kutumika kama waelimishaji rika ambao wanaweza kusambaza taarifa za afya na kutoa usaidizi kwa wenzao. Programu za elimu rika zinaweza kusaidia kukuza uaminifu na kuwezesha kushiriki habari ndani ya jamii.

5.1.6 Kukubalika na ufahamu

Kunaweza kuwa na ukosefu wa ufahamu miongoni mwa watoa huduma za afya na wateja kuhusu manufaa ya Utengamao Kidijitali. Upinzani wa kutumia teknolojia mpya au kushuku kuhusu ufanisi wake kunaweza kuzuia kukubalika na kuzitumia kama ilivyoelezwa katika jarida kutoka kwa Teriö na wengineo na Pandya na wengineo [12,14].

Ili kuondokana na kizuizi hiki kinachowezekana, mkakati wa kina unaweza kujumuisha:

Mafunzo na Kujenga Uwezo

Kutoa programu za mafunzo na warsha za kujenga uwezo kwa watoa huduma za afya, wahudumu wa afya ya jamii, na wataalamu wa utengamao ili kuimarisha uelewa wao wa teknolojia za Utengamao Kidijitali na ujumuishaji wao katika mazoezi. Kutoa uzoefu wa vitendo na usaidizi unaoendelea ili kuhakikisha umilisi na kujiamini.

Miradi ya Maonyesho na Majaribio

Utekelezaji wa miradi ya majaribio au programu za maonyesho kwa ushirikiano na vituo vya afya vya kijamii ili kuangazia ufanisi na athari zinazowezekana za Utengamao Kidijitali. Kusanya data na ushuhuda kutoka kwa washiriki ili kuonyesha manufaa na kujenga uaminifu ndani ya jumuiya.

Ushirikiano na Wadau Muhimu

Kuunda ushirikiano na mashirika ya serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, taasisi za kielimu, na makampuni ya teknolojia ili kutumia rasilimali, utaalamu, na mitandao kwa ajili ya kukuza ufahamu na kukubalika kwa Utengamao Kidijitali. Kushirikiana kwenye kampeni ili kukuza juhudi za utetezi na mipango ya kujenga uwezo.

Ujumbe na Nyenzo Zilizolengwa

Kutengeneza nyenzo za elimu zinazofaa kitamaduni, ikiwa ni pamoja na vipeperushi, mabango, video na maudhui ya mitandao ya kijamii, ili kueleza umuhimu wa huduma za Utengamao Kidijitali katika lugha za kiasili na miundo ya ndani inayoweza kufikiwa na hadhira mbalimbali. Zingatia hadithi za mafanikio na mifano ya ulimwengu halisi ili kutia moyo na kuhusisha dhana.

Utetezi wa Sera na Ushirikiano

Kutetea ujumuishaji wa Utengamao Kidijitali katika sera, mikakati na programu za kitaifa za huduma ya afya ili kurasimisha umuhimu wake na kupata ufadhili na usaidizi endelevu. Kushirikisha watunga sera na vikundi vya utetezi ili kutanguliza mipango ya huduma ya afya ya dijitali na kuondoa vizuizi vya udhibiti.

5.1.5. Ubunifu wa teknolojia

Usanifu duni wa huduma za utangamao, kama vile programu zilizoundwa vibaya, huathiri vibaya matumizi ya teknolojia. Hii ina maana, kwa mfano, ikiwa utumiaji haueleweki, mtumiaji lazima atumie muda fulani kujifahamisha na maudhui, na utendakazi, ambao utakuwa na athari mbaya katika kukubalika na wateja na wataalamu wa huduma za utengamao.

Muundo wa mfano, programu inapaswa kulengwa kwa watu wenye ulemavu wa kimwili. Kwa mfano, wateja wengi wanaohitaji huduma za utengamao wana matatizo ya kuona, ambayo yanazuia utumiaji wa simu janja/programu. Tatizo hili linaweza kutatuliwa kwa kutumia fonti kubwa na ikoni kwenye programu. Pia kunapaswa kuwa na njia ya wasioona kutumia programu kwa kupachika mwongozo wa sauti kwenye programu. Kwa mfano: Kwa kuwa tetemeko la watu walio na ugonjwa wa Parkinson ina shida ya kusogeza vidole vyao kimakusudi kwenye vitufe vya simu janjam, udhibiti wa sauti ungesaidia kutumia simu janja hata kama wana shida katika utendajikazi wao.

Ushirikiano 

Wakati makampuni, ambayo yanatengeneza vifaa vya kidijitali/huduma za utengamao, yatajumuisha wateja na wataalamu wa utengamao katika uundaji wa huduma hizi watapata taarifa muhimu kuhusu vipengele vya utumiaji. Kulingana na matokeo, kifaa/programu inaweza kubadilishwa zaidi, na utendaji mpya unaweza kuunganishwa. Kuhusisha kundi lengwa ni muhimu ikiwa tunataka watu wanufaike na huduma za Utengamao Kidijitali.

Miongozo ya Usanifu kwa Wote.

Miongozo pia ipo ili kubuni suluhu za kidijitali kuhusiana na hali halisi, ambapo watu wengi iwezekanavyo, bila kujali ulemavu, wanaweza kutumia kazi za jumla za uingiliaji kati. Soma sura ya 4 ili kujifunza zaidi kuhusu kanuni elekezi ya” Mwongozo wa Usanifu kwa Wote”, ambao unalenga kufanya malengo ya kidijitali kufikiwa na kila mtu licha ya changamoto za kimwili.

5.1.6. Sera na kanuni

Zaidi ya hayo, kukosekana kwa kanuni zinazohusiana na huduma za Utengamao Kidijitali kunaweza kusababisha vikwazo katika utekelezaji wake. Mfano halisi ni ukosefu wa uwazi juu ya taratibu za bili za huduma kama hizo – iwapo kampuni ya bima ya mteja inawajibika kwa malipo au wateja wanagharamikia wenyewe. Suala hili linachangiwa zaidi katika hali ambapo wateja hawana bima, na hivyo kuwa na changamoto ya ziada.

Mteja pia anaweza kujijeruhi wakati wa mazoezi akiwa nyumbani iwapo hayuko chini ya usimamizi. Pia hakuna kanuni kuhusu nani anawajibika na kubeba matokeo.

Kanuni mpya

Sera inahitajika ambayo inafafanua kwa usahihi masuala kama haya na kuandaa kanuni au kupitisha sheria ipasavyo ili kuwe na mbinu zinazowezekana za kutekeleza huduma za Utengamao Kidijitali kote nchini.