3.1 Mfumo wa Umilisi

Ili kutoa huduma bora za Utengamao Kidijitali, mtaalamu wa utengamao anahitaji umilisi mbalimbali [2] ili kutoa na kusaidia huduma za utengamao, zinazojumuisha sehemu za kidijitali na zisizo za kidijitali katika mchakato mzima wa huduma hizi.

Ili kuonyesha ni umilisi gani wa Huduma za Utengamao Kidijitali unaohitajika, Mfumo wa Umilisi wa Huduma za Utengamao Kidijitali katika Afrika Mashariki (MUHUK-Afrika Mashariki) uliundwa kama sehemu ya mradi wa RADIC. Mfumo huu unaainisha vipengele muhimu vya Huduma za Utengamao Kidijitali, kulenga kuboresha ufikiaji wa huduma za utengamao na kuimarisha ubora wa huduma katika kanda hii. Unashughulikia umilisi ulio muhimu, shughuli za kidijitali, na tabia zinazohitajika na wataalamu wa huduma ya utengamao ili kutoa na kusaidia huduma hizi ipasavyo, zinazojumuisha vipengele vya kidijitali na visivyo vya kidijitali katika mchakato mzima wa huduma za utengamao.

Mfumo huu umepangwa katika nyanja nne: afya, elimu, maisha na jamii, na uwezeshaji na unahusishwa na Mwongozo wa Kiashiria cha Huduma za Utengamao Jamii [3]. Nyanja hizi zinaelezea matokeo ya wataalamu wa huduma za utengamao kufanikiwa kupitia uingiliaji kati wa Huduma ya Utengamao Kidijitali. Ili kufikia matokeo, nyanja hizi zinaunganishwa na umilisi muhimu na kazi za kidijitali. Kwa madhumuni haya, vikoa vinne vya umilisi vimefafanuliwa na kueleza tabia ambayo mtaalamu wa huduma za utengamao anapaswa kuonyesha. Kwa hili, umilisi unakamilishwa na shughuli za wataalamu wa huduma za utengamao ambazo wanapaswa kufikia katika mchakato wa huduma hizi ili kupata mafanikio ya huduma za utengamao (wa kidijitali). Mfumo wa Umilisi wa Huduma za Utengamao Kidijitali katika Afrika Mashariki umekusudiwa kuongoza katika mafunzo na mazoezi.

MUHUK-Afrika Mashariki unatumika kwa taaluma na mipangilio yote ya huduma za utengamao katika Afrika Mashariki, unahudumia wateja wa marika yote wanaopokea huduma ya utengamao wa kimwili na kiakili. Mfumo huu uliundwa kupitia mchakato wa kurudiarudia unaohusisha maoni kutoka kwa wadau husika kama vile wataalamu wa huduma za utengamao, waelimishaji, na wanafunzi, pamoja na vyanzo vilivyotajwa.

Vyanzo vifuatavyo vilitumika katika maendeleo ya mfumo huu:

• Mwongozo wa Kiashiria wa Huduma za Utengamao Jamii [3]

• Mfumo wa Umilisi wa Huduma za Utengamao [4]

• UDi 2.2. - Mfumo wa Umilisi Dijitali kwa Wananchi [5]

• Tathmini ya mahitaji, ambayo ni matokeo ya uchunguzi wa mradi wa RADIC

• Uhakiki wa Mazingira, ambayo ni matokeo ya Mradi wa RADIC (kiungo kinakuja hivi karibuni)

Katika jedwali la 1, tunawasilisha nyanja nne zenye umilisi husika, umilisi muhimu na shughuli za kidijitali zinazohitajika na mtaalamu wa huduma za utengamao ili kufanya huduma hizi ziwe na mafanikio katika Afrika Mashariki. Jedwali hili linapaswa kutumika kwa maelezo ya jumla. Ikiwa unavutiwa na mfumo kamili, tumia kitabu cha waelimishaji (kinakuja hivi karibuni).

Competency Framework

Table 1. Dimensions, Definitions of Competencies, Key Competencies and digital activities in Digital Rehabilitation in East Africa.