7.1 Maadili katika mazingira ya Dijitali

Maadili ni tawi la falsafa linalofafanua kanuni bora, kama vile njia nzuri na za haki za kuishi na kutenda katika ulimwengu unaoshirikisha wengine. Maadili huongoza watu wakati wa kuchagua na husaidia kutathmini vitendo hata vya wengine. Pia husaidia katika kuchunguza sababu ya vitendo hivyo. Maadili hayatoi majibu yaliyo tayari, lakini hutoa zana za kutafakari na kufikiria.

Maadili katika Huduma ya Utengamao Kidijitali huhusisha matumizi ya kanuni katika uundaji, ustawishaji, utathmini, utekelezaji na utoaji huduma za teknolojia ya Huduma ya Utengamao Kidijitali. Kupuuza vipengele vya maadili kunaweza kusababisha hatari isiyotarajiwa kwa wateja na kusababisha kupungua kwa ufanisi, kutofuata sheria, na madhara, na hivyo kudhoofisha nia njema ya watoa huduma. Maadili ni muundo tata unaotumiwa wakati sheria na kanuni zinaruhusu uhuru wa maamuzi.

Wakati wa kujadili maadili katika Huduma ya Utengamao Kidijitali, unaweza kuzingatia mada katika muktadha wa afya kwa ujumla na kutazama mazoea ya kawaida ya maadili kwa simudawa [1]. Katika sura hii, tutajadili kanuni tano muhimu za maadili zilizowasilishwa awali katika muktadha wa simuafya lakini zimezingatiwa kwa uangalifu katika mwanga wa utengamao. Kanuni kuu ni uhuru, ukarimu, kutokuwa na madhara, haki na uhusiano wa mtaalamu na mgonjwa [2]. Kumbuka, kwamba wakati wa kujadili kanuni ya mwisho katika sura hii, neno 'mgonjwa' linabadilishwa na neno 'mteja'.

7.1.1 Uhuru

Kanuni ya kwanza, uhuru, ni kanuni kuu ya kimaadili ambayo inajumuisha kwa mfano uwezo wa mteja kufanya uchaguzi, kuwa na udhibiti, na kujiamulia. Wakati wa kutoa huduma zinazohusiana na afya dijitali, uhuru wa mteja unaweza kuboreshwa, kwa mfano, kuongeza uhuru wao wa kuishi maisha ya kujitegemea katika nyumba zao wenyewe, kukuza upatikanaji wa elimu na habari, na kupokea usaidizi kwa kiwango na wakati unaofaa zaidi, kwa wateja.  Hata hivyo, kuongezeka kwa uhuru unaotolewa na teknolojia kunaweza kusababisha kutengwa kwa wateja ikiwa wataachwa peke yao nyumbani, wakitegemea tu usaidizi wa kiteknolojia, na kukosa uwepo wa mlezi wa moja kwa moja. Ni muhimu wakati wowote inapowezekana kuweka kipaumbele uzingatiaji wa mahitaji na matakwa ya mteja, ikijumuisha kiwango chao cha uhuru wanachopendelea. Hivyo, ni muhimu kutafuta kibali cha ufahamu kutoka kwa wateja wakati wa kufanya maamuzi kuhusu utoaji wa huduma za dijitali, kwa maneno mengine, ili kuhakikisha kwamba wateja wanafahamu asili ya huduma zinazotolewa dijitali, ikiwa ni pamoja na mapungufu yao na hatari zinazoweza kutokea. Inapofaa na inapowezekana, mteja anapaswa kuwa na chaguo la kuchagua kati ya huduma za dijitali na za kitamaduni. Maswali kuhusu kuboresha uhuru si rahisi kwani mara nyingi huchukuliwa katika miktadha changamano na inayobadilika.

7.1.2 Ukarimu

Kanuni ya pili, ukarimu, inahusu kutenda mema au kutenda kwa manufaa ya wengine. Inamaanisha kuchukua hatua ili kukuza ustawi wa wateja, na inasisitiza kwamba wataalamu wanapaswa kutenda kwa manufaa zaidi ya wateja na kuzingatia ustawi wao katika kupanga na kutoa huduma. Huduma za dijitali zina uwezo wa kuwafaidi watu kwa kutoa uhakikisho, kuongeza imani katika kusimamia afya zao, kupunguza kutegemea walezi, kuboresha ufikiaji wa huduma bora za afya, na kuruhusu wateja kutibiwa katika mazingira yanayofahamika. Kanuni ya ukarimu inaweza kuboresha fursa za wateja kutenda kwa manufaa yao wenyewe na kuwezesha utoaji wa taarifa zinazosaidia ustawi wao.

7.1.3 Kutokuwa na madhara

Kanuni ya tatu ya maadili, kutokuwa na madhara, inasimamia kuzuia madhara. Katika muktadha wa utoaji wa huduma za dijitali, ni uwezekano kama vile kutumia muunganisho wa video au mbinu nyingine za ufuatiliaji ili kukagua wateja mara kwa mara ili kuhakikisha kuwa hakuna madhara yanayotokea katika mazingira ya nyumbani. Uwezekano wa wataalamu kuchagua kutoa huduma za mbali badala ya huduma zinazotolewa ana kwa ana katika hali ngumu au zenye mahitaji makubwa zinaweza kuwaweka wateja katika hatari na kuwahatarisha. Matumizi ya huduma za dijitali yanaweza pia kusababisha baadhi ya wateja kubebwa na majukumu zaidi, ambayo, kwa upande mwingine, yanaweza kuwawezesha wengine.

7.1.4 Haki

Haki, kanuni ya nne ya kimaadili, inasimamia usawa kuhusu ufikiaji sawa wa teknolojia, kwa kuzingatia mahitaji ya wateja, na kusawazisha yale yaliyo na mahitaji ya jamii pana. Faida kuu ya huduma za dijitali, ufikiaji wa huduma kwa jamii zilizotengwa, unaweza usifikiwe na wateja, jumuiya, au maeneo yenye rasilimali chache za kifedha au ujuzi wa dijitali. Kwa mfano, maeneo ya mbali yangehitaji na kufaidika na huduma za dijitali; hata hivyo, jamii hizo huenda zisiwe na uwezo wa kuzimudu, na katika hali nyingine, wateja wanaweza kukosa ujuzi unaohitajika wa kutumia teknolojia. Ni muhimu kuzingatia upatikanaji sawa, usambazaji wa haki wa teknolojia, na kuwepo kwa mgao wa dijitali wakati wa kuhusisha huduma za dijitali ili kuhakikisha haki katika huduma za utengamao. 

7.1.5 Uhusiano wa mtaalum na mteja

Kanuni ya tano ya maadili inajadili uhusiano wa mtaalamu na mteja. Wakati wa kuunda na kutekeleza huduma za digitali, ni muhimu kuzingatia aina na mazingira ya huduma ya utengamao, pamoja na mapendekezo ya mteja na uhusiano na mtaalamu.

Katika uwanja wa huduma za dijitali, huenda uhusiano ukavurugika. Ukosefu wa ukaribu wa kibinadamu unaonekana kuwa jambo la kusumbua, ingawa umuhimu wa ukaribu unaweza kutofautiana kati ya taaluma, tamaduni na watu mbalimbali. Zaidi ya hayo, uaminifu kati ya mteja na mtaalamu unaweza kudhoofishwa, haswa ikiwa wawili hawajawahi kukutana ana kwa ana. Kunaweza pia kuwa na mashaka yanayotokana na vifaa visivyojulikana na vile vile kusita kuzungumza wazi kupitia vifaa kwa sababu ya matatizo ya siri au mawasiliano.

Kwa upande mwingine, baadhi ya wateja wanaweza kupata mipangilio ya mawasiliano salama zaidi na kuhisi kuna uwezekano mkubwa wa kusikilizwa na wataalamu ikilinganishwa na hali ya mawasiliano ya ana kwa ana. Kuwasiliana kupitia suluhu za dijitali kunaweza kupunguza upweke kwa wateja ambao wangekuwa na mwingiliano mchache.

7.1.6 Mambo mengine ya kimaadili

Mbali na kanuni tano muhimu za maadili katika huduma ya afya, ulindaji wa siri na usiri wa taarifa za afya za mteja na kuhakikisha usalama wa teknolojia inayotumiwa katika utoaji huduma ni vipengele muhimu vya kuzingatia wakati wa kujadili maadili. Kwa mfano, suala la kimaadili linalohusiana na siri ya data linaweza kutokea wakati wateja wanapoombwa kujaza ukaguzi wa mtandaoni bila kufahamishwa kuhusu madhumuni ya utafiti na matumizi ya data iliyokusanywa. Teknolojia ya dijitali (kwa mfano, suluhu za mikutano ya video) pia hutoa nafasi za kibinafsi na ambapo wanafamilia wanaweza kuwepo. Katika hali hiyo, masuala ya siri na ushirikishwaji katika mchakato wa huduma za utengamao hupanuliwa ili kujumuisha watu wengine pamoja na wateja.

Wataalamu wanaohusika katika utoaji wa huduma za Utengamao Kidijitali lazima wawe na mafunzo ya kutosha ili kutoa huduma ya hali ya juu kwa kutumia teknolojia kwa ufanisi na usalama na kuhakikisha usalama wa mteja. Inapendekezwa pia kuwauliza wateja maoni kuhusu, miongoni mwa mengine, ufanisi wa huduma, uhusiano na mtaalamu, kukubalika kwa teknolojia na uvumbuzi, na mbinu zinazotumiwa katika huduma ya utengamao ili kuhakikisha ubora wa huduma. Zaidi ya hayo, wataalamu lazima wafuate sheria za serikali za mitaa, na jimbo, kanuni, na sera zinazosimamia huduma za dijitali zinazohusiana na huduma za utengamao na/au afya. Pata maelezo zaidi kuhusu Sera na Kanuni katika sura ya 7.2 na kuhusu Usalama wa Mtandao na Ulinzi wa Data katika sura ya 7.3.